mapishimapishi

mapishimapishi

Jumanne, 7 Januari 2014

MAGONJWA YANAYOTIBIWA KWA MATUMIZZI YA ASALI





1. Ugonjwa wa viungo/maumivu na uvimbe.
2. Kukatika kwa nywele.
3. Ukungu wa miguu.
4. Maambukizo kwenye kibofu cha mkojo.
5. Maumivu ya jino.
6. Lehemu (Cholestral).
7. Ugumba
8. Mchafuko wa tumbo.
9. Ugonjwa wa moyo
10. Shinikizo la damu.
11. Kinga ya mwili.
12. Ukosefu wa nguvu za kiume.
13. Flu.
14. Umri wa kuishi.
15. Chunusi.
16. Kuumwa na wadudu (kwa washawasha) wenye sumu.
17. Madhara ya ngozi.
18. Kupungua kwa uzito.
19. Saratani.
20. Uchovu mwilini.
22. Harufu mwilini.
23. Kupungua kwa usikivu.

SOMO LA LEO: UMUHIMU WA ASALI, FAHAMU ASALI HALISI NA FEKI, SOMA HAPA.


TUNAFAHAMU kwamba asali ina umuhimu mkubwa sana katika mwili wa binaadamu, lakini watu wengi wamekuwa wakipigwa kwa kuuziwa asali feki, sasa leo nimeona niwape darasa wanunuzi wa asali ili wasiweze kununua asali feki. 

Maana sehemu nyingi hasa Kariakoo, wafanyabiashara wamekuwa wakiuza asali ambayo haina ubora kwa kuchanganya maji na sukari guru. 
Njia ya kwanza, chukua njiti ya kibiriti kisha ichovye sehemu yenye baruti kwenye asali unayotaka kuinunua, kisha iwashe njiti hiyo kwa kutumia kibiriti chako, ikiwaka, ujue hiyo ni asali kweli. 
Njia ya pili, dondosha asali chini katika mchanga, ukiona sehemu ya mchanga iliyolowana ikijikusanya pamoja ujue hiyo nii asali orginal. 
Njia ya tatu, Chukua karatasi jeupe, dondoshea asali njia juu yake, kama ikichelewa kutokea upande wa pili, ujue hiyo asali safi na inafaaa kwa matumizi ya binaadamu.
Bado kuna njia nyingine ambayo hutumiwa na baadhi ya watu, kama vile kuimwaga katika kiganja cha mkono wako, ukiona tone la mwisho linabakia kwenye chupa kuja mkononi, hiyo ni asali nzuri. 
Pia wengine huangalia kama ikiwa kwenye chupa huwa inatengeneza alama yenye mfano wa korosho. 
Nadhani hutaibiwa tena kwa kuuzia asali feki.


Jumatatu, 6 Januari 2014

NAMNA YA KUANDAA MISHKAKI YA MAANDAZI

Napenda sana kupika maandazi,kila ninapokanda unga wa maandazi nahisi kama ninashika udongo mfinyazi na akili yangu uwaza kubumba,kukata na kutengeneza vitu au maumbo mbalimbali.
031
Mishkaki ya maandazi  ni kama maandazi mengine yoyote chatofauti nikwamba maandazi haya huwekwa kwenye mti au mdenge wa mshkaki nahivyo hufanana sana na mshkaki
Unaweza andaa maandazi haya kwakutumia recipe yoyote ya maandazi unayopenda.Chagua recipe yoyote yamaandazi hapa jikoni.
Njia
1.Kanda unga wa maandazi  adi uwe tayari kwa kusukuma
2.Gawanya unga wako mara nne zaidi kutokana na wingi wake,kisha sukuma ili kupata chapati nene
  • Chapati ikiwa nyembamba ,ukikaanga maandazi yatajaa hewa ndani na yatachomoka kwenye mti /mdenge wa mshkaki
3.kwakutumia kisu kikali kata unga wako katika vipande virefu vyembamba (kwa urefu).kisha chukua kipande kimoja na ukikate vipande vidogo vidogo (kwa upana) .Utapata maandazi madogo madogo katika umbo la pembe nne.
018
4.Pakaa unga wa ngano kwenye mti wa mshakaki ,kisha Chomeka maandazi hayo kwenye mti huo  uku ukuicha nafasi yakutosha kila baada ya andazi moja ili kutoa nafasi ya andazi kuumuka wakati wakukaanga .
5.Kaanga kama unavyokaanga maandazi kawaida.Weka kwenye chujio yadondoshe mafuta kisha weka juu ya chombo kilichotandikwa karatasi ili kuondoa mafuta yaliobaki juu.Maandazi tayari kwa kula.
Muonekano wa maandazi haya huvutia sana. Ni vyema kua na utofauti katika upishi wako,mpe mlaji kitu chakushangaa na kufuraia anapokula.
Naamini ukiandaa maandazi haya siku yakwanza familia yako itakua na mengi yakusema.kama mtoto hawapendi kula basi hii ni namna nyingine yakumvutia mtoto kula.

MUONEKANO MZURI WA CHAKULA HUMVUTIA MLAJi

Ijumaa, 3 Januari 2014

EBWANA EHHH!!!!!TAZAMA PICHA ZA MGAHAWA MAALUMU ULIOFUNGULIWA KWA AJILI YA PAKA NA MBWA,JIONEE MBWA AKIFANYA ODA YA CHAKULA

Mgahawa wa kwanza maalum kwaajili ya mbwa na paka uitwao ‘Pets Deli’ umefunguliwa huko Berlin, Ujerumani.
Pets deli-1
Kati ya vyakula vinavyopatikana katika menu ya mgahawa huo ni pamoja na beef, bata mzinga, cupcakes, wali, viazi bila kusahahu nyama ya Kangaroo.
Pets deli-2
Mgahawa huo uliofunguliwa katika kipindi cha Christmas mwaka jana 2013, vyakula vya wanyama hao vinauzwa kuanzia €3 hadi €6 (6500-13000Tsh).
Pets deli-3
Katika mgahawa huo kuna sehemu imetengwa kwaajili ya wamiliki wa wanyama hao kupata kahawa wakisubiri mbwa na paka wao wapatiwe huduma.
Pets deli-4
Pets deli-5
Mmiliki wa mgahawa huo David Spanier (31) alisema alipata wazo baada ya kugundua rafiki yake hua anashindwa kutumia vyakula vya supermarket kwaajili ya wanyama kutokana na kuwa junk food.

Pets deli-6
Spiner aliongeza kuwa nyama inayoandaliwa ina ubora ambao inaweza hata kuliwa na binadamu bila tatizo.
Pets deli-7



Jumatatu, 23 Desemba 2013

TAZAMA PICHA ZA MPISHI HUYU WA AJABU DUNIANI ANAYECHOMA KUKU KWA KUTUMIA MOTO UNAOTOKA KWENYE GARI AINA YA LAMBORGHINI



This is the moment a Christmas turkey was roasted on the world's most expensive cooker - a £300,000 Lamborghini.
Car blogger Tim Burton, from London, bought a fresh turkey and put the festive bird on the end of a pitchfork.
He then bravely stood behind the 700bhp Lamborghini Aventador and got the owner of the supercar to rev as hard as he could.

Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Inferno: Car blogger Tim Burton bought a fresh turkey and put the festive bird on the end of a pitchfork

Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Ready to eat! The browned turkey was roasted in 10 minutes but this method is unlikely to replace the oven


As the Italian motor reached a whopping 9,000 revs, huge flames spewed from its exhaust - blasting the turkey with extreme heat.
 


Mr Burton, who makes YouTube videos under the name Shmee150, stood while the bird was given the alternative Christmas roasting for more than ten minutes.
The result was a browned turkey - although the high octane method is unlikely to replace the oven around the country any time soon.
Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Danger: The bird is placed near the engine before the owner revs with Mr Burton just inches from the flames
Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Heat: Mr Burton stood behind the 700bhp Lamborghini Aventador and got the owner of the supercar to rev


Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Extreme: As the Italian motor reached a whopping 9,000 revs, huge flames spewed from its exhaust


Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Expensive: The £300,000 car which was used for the cooking experiment - but is better suited to driving


He said: 'It is a standard Christmas ritual that I collect the turkey for our family lunch and this year I thought I'd try a new way to cook it.
'I'm not sure I'd recommend this though unless you enjoy the taste of exhaust gases.'


Alhamisi, 19 Desemba 2013

Lishe ya Mtoto: Miezi 6-12


Kwa miezi sita ya kwanza katika maisha ya mtoto chakula pekee ambacho wataalamu wa afya wanashauri apewe ni maziwa ya mama tu. Kunyonyesha ndio njia ya kwanza kabisa kumpa mtoto chakula. Unapoanza kumpa mtoto vitu vingine kama maziwa ya kopo wakati ana miezi michache utoaji wako wa maziwa unaathirika maana jinsi mtoto anavyonyonya ndivyo jinsi maziwa yanavyotengenezwa ndio maana watu wengi wanavyoanza kazi na kumuacha mtoto nyumbani maziwa yao yanaanza kupungua. Faida za kunyonyesha maziwa ya mama ni pamoja na:
  1. Maziwa ya mama yana virutubisho vingi vya asili ambavyo ni muhimu sana katika ukuaji na kinga kwa mtoto. Humlinda na magonjwa mengi ya utoto pamoja na ‘allergies’ mbalimbali.
  2. Hukuwezesha kuwa na ukaribu na mtoto wako.
  3. Hukupunguzia uwezekano wa kupata kansa ya matiti.
  4. Ni bure na unaweza kumpatia maziwa wakati wowote bila usumbufu.
Wakati gani Uanze Vyakula Vingine
Mtoto wako akifikisha miezi 6 unaweza kuanza kumpatia vyakula vingine kidogo kidogo ( Kuna ambao kutokana na sababu Fulani daktari huwashauri kuanza mtoto akiwa na miezi 4 hivyo ni  vyema ukiwasiliana na daktari wako kwanza). Mtoto akianza kupewa vyakula nje ya maziwa mapema kabla ya miezi 4 ni hatari kwa afya yake maana mfumo wake wa kusaga chakula unakuwa bado haujawa tayari. Unapoanza kumpa vyakula vingine hauachi kumnyonyesha, unyonyeshaji unaendelea hadi miaka miwili na nusu.
Dalili kuwa mtoto wako yupo tayari kuanza vyakula vingine ni:
  1. Amefikisha miezi 6
  2. Anaweza kushikilia kichwa juu ( shingo imekaza)
  3. Anaweza kukaa kwa kuwekewa kitu ( mfano kiti chenye mkanda)
  4. Unapompa chakula na kijiko anafungua mdomo kutaka kupokea au anageuza uso kwa kukataa
  5. Akipokea chakula anakiweka mdomoni na kujaribu kumeza na sio kukisukuma nje na kuacha mdomo wazi.
Hakikisha mtoto wako yupo tayari kabla hujaanza kumpa chakula na usimlazimishe sana anapoanza maana anaweza kuchukia chakula, inawezekana hapendi chakula ulichompa jaribu kubadilisha uone anapenda nini. Kila mtoto ni tofauti na mwingine hivyo usimlinganishe mtoto wako na mwingine la muhimu ni kuhakikisha kuwa anauzito kulingana na umri wake na anaongezeka kwa kupanda chati.
Mnapokuwa mnakula mezani mtoto naye awe hapo ili kumpa hamu ya kula na sio kila wakati akila anakuwa peke yake. Mpe chakula akiwa na furaha na pia akiwa na njaa ili aweze kufurahia chakula chake. Kabla ya kubadilisha aina ya chakula mpe kwa siku 3-4 mfululizo ili aweze kukizoea na kama kitamletea madhara ujue hasa ni chakula gani. Usimchanganyie vyakula maana hutajua anapenda nini na kuchukia nini na pia kama kuna kitu kitamdhuru ukichanganya hautagundua kwa urahisi.
Miezi 6-9
Endelea kunyonyesha na anza kumpa vyakula vyenye madini ya chuma. Mtoto alishwe kwa ratiba inayoeleweka kila siku na katika ratiba hiyo hakikisha angalau mara moja kwa siku muda wake wa kula unakuwa sawa na muda wa familia yote ili muweze kula pamoja. Vyakula vyake viwe vimepondwapondwa kabisa ikiwezekana tumia blender na hakikisha anapata mlo kamili yani matunda, mbogamboga, mbegu, nafaka, nyama na samaki. Inashauriwa kutokuchanganya aina tofauti za nafaka kwenye unga mmoja unapomtengenezea uji, uwe na unga wa mahindi, ulezi,mchele n.k tofauti tofauti. Pika aina moja ya uji kwa wakati unaweza kufanya kwa wiki au vyovyote utakavyopenda.
 Unapompa mboga au matunda anza na tunda moja moja kwa wakati. Osha vizuri matunda yako na katakata vizuri na kuponda ponda kisha mpe kiasi kidogo kwa wakati na kikibaki usikiweke, mtengenezee kile atakachokula tu. Matunda kama papai, parachichi na embe ni mazuri kwa kuanzia. Chemsha maharage, njegere au mboga za majani na kumpa supu kidogo kidogo, usiweke chumvi nyingi kidogo sana inatosha. Usimpe juisi za madukani, hakikisha unamtengenezea juisi wewe mwenyewe na usichanganye matunda mbalimbali kwenye juisi moja, na usiweke sukari kabisa.
Miezi 9-12
Katika umri huu mtoto anakuwa tayari amezoea ladha tofauti tofauti za vyakula mbalimbali nje ya maziwa. Anauwezo wa kukaa na kushikilia kitu kwa mikono yake na kuweka mdomoni hivyo anza kumpa matunda laini mkononi aanze kujifunza kula mwenyewe. Hakikisha vipande sio vidogo sana anavyoweza kumeza ili kuepuka hatari ya kukabwa. Kwa sababu pia atakuwa ameanza kuota meno atakuwa anapenda sana kutafuna tafuna. Katika umri huu pia unaweza kuanza kumpa kiini cha yai, ute wa yai hadi afike umri wa mwaka mmoja. Endelea kumnyonyesha ila kwa sasa anakula kwanza kisha ndio ananyonya maana akinyonya sana anaweza akakataa chakula. Usimpe chakula kimoja mfululizo kwa muda mrefu maana atakinai na kuanza kukataa chakula, mpe vyakula tofauti tofauti ili aendelee kupenda chakula.
Jinsi ya Kutengeneza Chakula cha Mtoto
Ni rahisi sana kutengeneza chakula cha mtoto nyumbani kwako. Osha mikono yako vizuri kabla ya kuandaa chakula na hakikisha unatumia vyombo visafi.
Matunda na mboga mboga: osha mboga zako vizuri kwa maji safi ( ya uvugu vugu) na kisha katakata na kubandika jikoni kwa chumvi kidogo sana bila mafuta. Ikichemka isage kwenye blender au ponda ponda iwe laini kabisa kisha mpe mtoto. Matunda osha pia kwa maji ya uvugu vugu, toa ganda la nje na kata vipande vikubwa kama unataka ale kwa mikono yake mwenyewe au ponda ponda na upe kwa kijiko.
Nyama na Samaki: Chemsha vipande vya nyama na maji kidogo na iive kwa moto wa kiasi hadi ilainike kabisa kisha isage kwenye mashine (food processor) na umpe na ile supu. Samaki vile vile ila samaki hakuna haja ya kuisaga maana ikiiva inalainika sana na ni rahisi kwa mtoto kula bila taabu (Kuwa makini sana na mifupa!).
Mbegu: Hapa nazungumzia maharage, kunde, choroko, njegere n.k Pika hadi ziive kabisa na kulainika kisha pondaponda na kumpa mtoto. Pia viazi na ndizi vinafaa sana kwa watoto, unaweza ukachanganya na supu ya samaki / nyama au na maziwa.
Nafaka: Usichanganye nafaka tofauti tofauti kwa ajili ya uji wa mtoto, inashauriwa kuwa na unga tofauti kwa kila nafaka. Unapopika uji unaweza kuweka karaga zilizosagwa ili kuongeza mafuta na vitamin kwenye lishe ya mtoto.
Usalama katika Kula
  1. Hakikisha haumuachi mtoto mdogo na chakula au kinywaji bila uangalizi hata kama ni maziwa ya chupa asije akapaliwa. Usimpe mtoto chakula au maziwa akiwa amelala, analia au anacheka.
  2. Usimpe chakula ambacho kinaweza kumkaba au kumpalia kama karanga, maindi, zabibu n.k
  3. Kabla ya kumpa mtoto chakula hakikisha umekiangalia joto lake usije ukamuunguza mdomo.
  4. Usafi wa mtayarishaji, mlishaji na mlishwaji ni muhimu san asana.
Mfano wa Ratiba ya Mlo wa Mtoto
Ratiba hii ni ya mfano tu, vyakula vilivyotenganishwa na / inamaana nikimojawapo kati ya hivyo. Hakikisha vyakula havichukui nafasi ya maziwa maana ni ya muhimu kwa afya ya mtoto wako.

MUDA MIEZI 6 – 9 MIEZI 9 – 12
Alfajiri (saa 11-12) Maziwa ya mama Maziwa ya mama
Asubuhi (saa 1-2) Maziwa ya mamaUji ( Cerelac)
Tunda la kupondwa pondwa
Maziwa ya mamaUji ( Cerelac)
Tunda la kupondwa pondwa
Kabla ya mchana (saa 4-5) Maziwa /  Kipande cha mkateMaji Maziwa / andazi / chapatti laini / Kiini cha yaiMaji
Mchana (saa 6-7) Ndizi / Viazi / Wali vya kupondwa pondwaSupu ya mboga ya majani / mbegu / samaki / nyama
Tunda la kupondwa pondwa
Ndizi / Viazi / Wali / UgaliMboga za majani / Nyama / Mbegu / Samaki
Kipande cha Tunda
Alasiri ( Saa 9-10) Maji Maji
Jioni (saa 12-1) Uji / CerelacSupu ya mboga / mbegu / nyama / samaki Uji / CeleracMboga / Mbegu / Nyama / Samaki
Usiku ( muda wowote) Maziwa Maziwa

JIFUNZE KUTENGENEZA KWA UMARIDADI NA UFASAHAA KIFUA CHA KUKU




MAHITAJI
1 kijiko kidogo cha chai Kosher Salt
1 kijiko kidogo cha chai Freshly Ground Black Pepper
1 kijiko kidogo cha chai Onion Powder
1 kijiko kidogo cha chai Garlic Powder
1 kijiko kidogo cha chai Dried Parsley Flakes
Na Chef Issa Kapande
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Changanya viungo vyote kwa mara moja kisha mwagia juu ya vifua vya kuku

Ukitaka upate harufu na ladha safi toka katika viungo hivi hakikisha umeasha moto na kikaango kipate moto wa kutosha kisha mwagia mafuta yakupikia yakutosha na mwagia pia viungo vilivyobakia kwenye kikaango kisha weka hivyo vifua vyakuku na upunguze moto uwe wa wastani.

Chukua mfuniko funika ila acha wazi kiasi kama muonekano kwenye picha lengo ni kupunguza mvuke isiwe kama tunachemsha badala ya kukaanga. Kaanga kwa dakika 3 kisha geuza upande wa pili uweze pata rangi ya kahawia nzuri.
 
Baada ya kugeuza upande wa pili huu ndio muonekano wake na kisha pika pia kwa dakika 3 na kifua cha kuku kitakua kimeiva. Kumbuka unapogeuza upande wa pili toa na mfuniko usifunike tena.

Huu ni muonekano wa perfectly cooked and seasoned chicken breast baada ya kukata ndani inakua laini na ladha safi kabisa sio kau kau na kupoteza ladha.


KIfua hiki cha kuku mimi na familia yangu tulikula na mchanganyiko wa parachici, slice za vitunguu, slice za nyanya mbivu limao na giligilani mhhhhhh safi sana.
 
NDANI YA DAKIKA 10 CHAKULA TAYARI