mapishimapishi

mapishimapishi

Jumapili, 15 Septemba 2013

JIFUNZE JINSI YA KUPIKA MKATE HUU MWEUPE


JIFUNZE KUTENGENEZA MKATE HUU MWEUPE NI RAHISI NA NAFUU KUANDAA ONYESHA UJUZI WAKO KATIKA FAMILIA
 
MAHITAJI
 
1 kg unga wa ngano
2 kijiko kidogo cha chai chumvi
240 gram maziwa ya maji ya vugu vungu
60 gram maji ya vugu vugu
2 kijiko kikubwa cha chakula siagi, iyeyushe
3 kijiko kikubwa cha chakula asali
2 kijiko kidogo cha chai amira ya chenga

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
Muda wa maandalizi : Masaa 2 hadi 4
Muda wa mapishi : Dakika 30 hadi saa 1
Idadi ya walaji : Watu 4
Ujazo : Unapata mkate wenye 9-inch
 
 
Chukua robo tatu ya unga pamoja na chumvi kisha chukua mchapo na uchanganye. 

 
 Chukua bakuli safi kavu kisha changanya maziwa, majina, siagi, chumvi pamoja na amira. Hakikisha joto la maziwa na maji liwe 110 degrees.

 
 Mimina mchanganiko wako wenye maziwa katika unga.

 
Anza kukanda pole pole 

 
Hapa mchanganyiko wako umeshaanza kushikana. 

 
Chukua mchanganyiko wako kisha weka juu ya meza hakikisha umemwagia unga kwa juu endelea kukanda vizuri kwa dakika 10.

 
Kama unafikiri mchanganyiko bado una maji maji, basi chukua robo ya unga iliobakia tumia kijiko kikubwa cha chakula ongeza kimoja kimoja epuka kuweka unga wote ukazidisha.

 
Chukua bakuli safi na kavu, kisha lipake mafuta na weka mchanganyiko wako katika hiyo bakuli. 

 
KIsha tumia plastic na funika weka sehemu yenye joto, jikoni kuna joto.

 
Hakikisha mchanganyiko wako umeongezeka mara 2, ndani ya dakika 40 mpaka 50. 

 
Kisha chukua mchanganyiko wako ukande vizuri na weka katika chombo chako cha kuokea kiwe cha chuma au cha kioo kama changu chenye ukubwa wa  8.5 X 4.5 X 2.5 (1.5 Lita).

 
 Kisha funika tena kwa plastic

 
 Weka pembeni kwa dakika 20 mpaka 30 itakua imeshaumuka vizuri kama unavyoona katika picha weka katika oven.

 
 Kumbuka oven yako unatakiwa uiwashe kabla katika joto la 350 degrees, ukishaweka unga katika oven unaweza rushia maji kidogo ili kuweka mvuke utakao saidia kuweka rangi nzuri ya brown na kua na gamba gumu. Oka kwa dakika 40 mpaka 50 mkate wako utakua umeiva.

 
Toa mkate wako katika pan, hamishia katika wire rack, ili mkate uweze kupoa.

 
Kata kata vipande na wapatie walaji, unaona mkate ulivyochambuka. 

 
Unaweza ukavuta picha huu mkate ni mtamu kiasi gani ukishapaka siagi kwajuu? au ukipaka jam pia? Ni mtamu sana sana.
  kwa msaada wa activechef blog

JIFUNZE KUPIKA YA MUFFIN YENYE MCHANGANYIKO WA VIPANDE VYA CHOCOLATE NA KARANGA


 
RECIPE SAFI KABISA YA MUFFIN YENYE MCHANGANYIKO WA VIPANDE VYA CHOCOLATE NA KARANGA NI TAMU RAHISI NA NI NAFUU KUANDAA

MAHITAJI

250 gram siagi laini
250 sukari
2 mayai
250 gram plain yogurt
1 kijiko kidogo cha chai vanilla
500 gram  unga wa ngano
1 kijiko kidogo cha chai baking soda
1/2 kijiko kidogo cha chai baking powder
1/2 kijiko kidogo cha chai chumvi
180 gram vipande vya chocolate
1 kijiko kidogo cha chai cinnamon powder
4 kijiko kikubwa cha chakula karanga za kuoka
2 kijiko kikubwa cha chakula sukari ya brown
60  gram vipande vya chocolate
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
Muda wa maandalizi : Dakika 30
Muda wa mapishi : Dakika 30
Idadi ya keki : 12 Muffins
 
Katika bakuli changanya sukari na siagi pamoja.
 
Kisha mimina mayai pole pole endelea kuchanganya katika mchanganyiko wa sukari na siagi.
 
Kisha ongeza yogurt na vanilla na uchanganye ichanganyike vizuri.
 
Kisha chukua bakuli safi na uchanganye unga wa ngano pamoja na baking soda, baking powder na chumvi.
 
Kisha chukua mchanganyiko wa unga kisha mimina polepole katika mchanganyiko wa mayai.
 
Kisha mimina vipande vya chocolate na uendelee kuchanganya polepole.
 
KIsha chukua tray ya kuokea na weka vikombe vya karatai kisha mimina mchanganyiko wako 2/3 hakikisha isijae kabisa.
 
Kisha chukua bakuli kavu weka vipande vya chocolate vilivyobakia, cinnamon powder na karanga changanya pamoja.
 
Kisha mwagia kwa juu mchanganyiko huo kwenye tray ya kuokea izibe ile nafasi iliyobakia.
 
Hakikisha oven unaiwasha dakika 5 kabla ya kuoka Choma katika ovena katika moto wa 350F kwadakika 20 had 30. Poza keki zako kwa dakika 5 kabla ya kuzitoa katika pan.
 
Naimani ukizieweka sehemu nzuri ukafunika safi zisiguswe na wadudu zinaweza kukaa kwa siku tatu bila ya kuharibika!
 
 WAANDALIE FAMILIA AU WATEJA WAKO WAFURAHIE.
  kwa msaada wa activechef blog

JIFUNZE KUPIKA SAMAKI KATIKA OVEN KWA KUTUMIA FOIL


 
NI RAHISI, NAFUU NA HARAKA SANA KUANDAA AINA HII YA MAPISHI YA SAMAKI KWA KUTUMIA FOIL NA KUOKA KATIKA OVEN LAKINI SAMAKI ATATOKA KAMA AMECHEMSHWA NA AKIWA NA LADHA SAFI SANA BILA YA KUPOTEZA VIRUTUBISHO VYOTE MUHIMU.
 
MAHITAJI
1pc kitunguu maji kikubwa
1 pc limao kubwa
5 gram binzali
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
1 pc pili pili hoho kubwa
50 gram tomato pest ( nyanya ya kopo)
kipande cha foil kutokana na ukubwa wa samaki
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
 
Huu ni muonekano wa samaki akiwa mbichi tayari umeshamsafisha vizuri kwa maji baridi na mapishi haya unaweza tumia kwa samaki aina ya sato, sangara, kibua, change, jodari au kole kole na akaiva na ladha safi kabisa.

 
Katika picha unaona mchanganyiko wa vitunguu, pilipili hoho, maji ya limao, binzali, chumvi, pili pili manga na nyanya ya kopo baada ya kuchanganya pamoja kasha mpakae samaki pande zote mbili ulizompasua ili mchanganyiko huu uingie vizuri katika nyama kasha mabaki ya huo mchanganyiko mjazie tumboni kisha mfunike vizuri na foil muweke katika oven tayari ikiwa na moto.
 
Jana mchana niliporudi nyumbani niliandalia samaki aina ya sato pamoja na maharage ya Nazi na ugali wa mahindi nipo ulaya lakini na kula chakula nilichokizoea nyumbani Tanzania na kwa ladha na ubora ule ule.
 
 
 
Unaweza kumpika katika oven kwa dakika 30 kwenye moto wa degree 200 hadi 250 pia kwa mtindo huu unaweza kumchoma katika jiko la mkaa akiwa hivi hivi katika foil na akaiva safi kabisa
 
 
 
Baada ya nusu saa samaki wako atakua ameiva na atakua na muonekano kama huu na ladha safi sana
 

 
Hapa sasa ndio nilikua namfunua vizuri tayari kwa chakula cha mchana

 
Hata kama samaki amekaa kwenye friza kwa muda mrefu mchanganyiko huu wa mboga majani limao na viuongo vinasaidia sana kuamsha ladha ya samaki wako pika familia ifurahie.
kwa msaada wa activechef

Jumatano, 28 Agosti 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA KUKU WA KUKAANGA PAMOJA NA CHEESE NA SAUCE SAFI


 
KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA KUKU HUYU WA KUAANGA PAMOJA NA CHEESE NA UNGA WA MIKATE
 
MAHITAJI
 
240 gram shredded Parmesan cheese
3 vifua vya kuku
480 gram unga wa mkate wa kahawia au bread crumbs
100 gram Italian seasoning, nitakuelekeza jinsi ya kuitengeneza
240 gram sauce aina ya ranch
1 lita ya mafuta kwa kukaangia
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
 
JINSI YA KUANDAA FATILI APICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
 
 

 


 

 

 

 

JIFUNZE KUTENGENEZA WALI WA MCHANGANYIKO WA NYAMA YA KUKU NA CHEESE


 
KAA TAYARI KUJIFUNZA KUTENGENEZA WALI WA MCHANGANYIKO WA NYAMA YA KUKU NA CHEESE
 
NAOMBA RADHI KWA KUA KIMYWA KWA MUDA HII NI KUTOKANA NA MAJUKUMU LEO JIONI NITAJITAIDI NIWEKE MAELEZO YA VYAKULA VYOTE VISIVYO NA MAELEZO HAPA KATIKA BLOG
 
MAHITAJI  
4 vifua vyakuku (kata kata vipande vidogo)
 360 gram ya maji
1 kijiko kikubwa cha chakula graham masala
1 nyanya ya kopo
500gram sawa na nusu kilo ya mchle
240 gram shredded cheddar cheese
1 kopo la mtindi halisi usio na ladha
1 parachichi au avocado safi lilioiva
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAEEZO HAPOCHINI
 
 







 
 

Jumatano, 24 Julai 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA HOT CHOCOLATE YA MCHANGANYIKO NAZI

 
KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA MUDA SI MREFU
 
MAHITAJI
 
500gram low fat Milk yanapatikana duka lolote la chakula
200gram tui la nazi
60 gram maziwa ya kawaida yaliyochemshwa yakapoa
1 kijiko kikubwa cha chakula Cocoa powder
1/4 kijiko kidogo cha chai Vanilla
50 gram fresh whipped cream (sio lazima)
vipande vya Chocolate (sio lazima)
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Muda wa maandalizi Dakika 15
Muda wa kutengeneza: Dakika 15
Idadi ya walaji: Watu 3
Ujazo baada ya kuandaa : 600 ml

 
Katika kikaango mimina maziwa aina zote pamoja na tui la nazi.

 
Chemsha mchanganyiko huu kwa moto mdogo, hakikisha unakoroga pole pole.

 
Kisha mimina unga wa cocoa  na uendelee kukoroga

 
Hakikisha unaendelea kukoroga ichanganyike vizuri.

 
Toa katika moto kisha mimina vanilla katika mchanganyiko wako.

 
Mchanganyiko wako utakua mziko kiasi mpatie mnywaji  ikiwa ya moto juu yake unaweza pamba na whipped cream pamoja na unga wa chocolate. Hutaweza kusikia ladha kali ya nazi ila kama wewe ni mpenzi sana wa nazi punguza idadi ya maziwa kisha weka nazi zaidi kwa ladha unayotaka. Muandalie mgeni nyumbani au watoto kinywaji hiki rahisi na cha haraka kuandaa.