mapishimapishi

mapishimapishi

Jumatatu, 23 Desemba 2013

TAZAMA PICHA ZA MPISHI HUYU WA AJABU DUNIANI ANAYECHOMA KUKU KWA KUTUMIA MOTO UNAOTOKA KWENYE GARI AINA YA LAMBORGHINI



This is the moment a Christmas turkey was roasted on the world's most expensive cooker - a £300,000 Lamborghini.
Car blogger Tim Burton, from London, bought a fresh turkey and put the festive bird on the end of a pitchfork.
He then bravely stood behind the 700bhp Lamborghini Aventador and got the owner of the supercar to rev as hard as he could.

Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Inferno: Car blogger Tim Burton bought a fresh turkey and put the festive bird on the end of a pitchfork

Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Ready to eat! The browned turkey was roasted in 10 minutes but this method is unlikely to replace the oven


As the Italian motor reached a whopping 9,000 revs, huge flames spewed from its exhaust - blasting the turkey with extreme heat.
 


Mr Burton, who makes YouTube videos under the name Shmee150, stood while the bird was given the alternative Christmas roasting for more than ten minutes.
The result was a browned turkey - although the high octane method is unlikely to replace the oven around the country any time soon.
Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Danger: The bird is placed near the engine before the owner revs with Mr Burton just inches from the flames
Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Heat: Mr Burton stood behind the 700bhp Lamborghini Aventador and got the owner of the supercar to rev


Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Extreme: As the Italian motor reached a whopping 9,000 revs, huge flames spewed from its exhaust


Moment Christmas bird is roasted on the world's most expensive cooker... a £300,000 LAMBORGHINI
Expensive: The £300,000 car which was used for the cooking experiment - but is better suited to driving


He said: 'It is a standard Christmas ritual that I collect the turkey for our family lunch and this year I thought I'd try a new way to cook it.
'I'm not sure I'd recommend this though unless you enjoy the taste of exhaust gases.'


Alhamisi, 19 Desemba 2013

Lishe ya Mtoto: Miezi 6-12


Kwa miezi sita ya kwanza katika maisha ya mtoto chakula pekee ambacho wataalamu wa afya wanashauri apewe ni maziwa ya mama tu. Kunyonyesha ndio njia ya kwanza kabisa kumpa mtoto chakula. Unapoanza kumpa mtoto vitu vingine kama maziwa ya kopo wakati ana miezi michache utoaji wako wa maziwa unaathirika maana jinsi mtoto anavyonyonya ndivyo jinsi maziwa yanavyotengenezwa ndio maana watu wengi wanavyoanza kazi na kumuacha mtoto nyumbani maziwa yao yanaanza kupungua. Faida za kunyonyesha maziwa ya mama ni pamoja na:
  1. Maziwa ya mama yana virutubisho vingi vya asili ambavyo ni muhimu sana katika ukuaji na kinga kwa mtoto. Humlinda na magonjwa mengi ya utoto pamoja na ‘allergies’ mbalimbali.
  2. Hukuwezesha kuwa na ukaribu na mtoto wako.
  3. Hukupunguzia uwezekano wa kupata kansa ya matiti.
  4. Ni bure na unaweza kumpatia maziwa wakati wowote bila usumbufu.
Wakati gani Uanze Vyakula Vingine
Mtoto wako akifikisha miezi 6 unaweza kuanza kumpatia vyakula vingine kidogo kidogo ( Kuna ambao kutokana na sababu Fulani daktari huwashauri kuanza mtoto akiwa na miezi 4 hivyo ni  vyema ukiwasiliana na daktari wako kwanza). Mtoto akianza kupewa vyakula nje ya maziwa mapema kabla ya miezi 4 ni hatari kwa afya yake maana mfumo wake wa kusaga chakula unakuwa bado haujawa tayari. Unapoanza kumpa vyakula vingine hauachi kumnyonyesha, unyonyeshaji unaendelea hadi miaka miwili na nusu.
Dalili kuwa mtoto wako yupo tayari kuanza vyakula vingine ni:
  1. Amefikisha miezi 6
  2. Anaweza kushikilia kichwa juu ( shingo imekaza)
  3. Anaweza kukaa kwa kuwekewa kitu ( mfano kiti chenye mkanda)
  4. Unapompa chakula na kijiko anafungua mdomo kutaka kupokea au anageuza uso kwa kukataa
  5. Akipokea chakula anakiweka mdomoni na kujaribu kumeza na sio kukisukuma nje na kuacha mdomo wazi.
Hakikisha mtoto wako yupo tayari kabla hujaanza kumpa chakula na usimlazimishe sana anapoanza maana anaweza kuchukia chakula, inawezekana hapendi chakula ulichompa jaribu kubadilisha uone anapenda nini. Kila mtoto ni tofauti na mwingine hivyo usimlinganishe mtoto wako na mwingine la muhimu ni kuhakikisha kuwa anauzito kulingana na umri wake na anaongezeka kwa kupanda chati.
Mnapokuwa mnakula mezani mtoto naye awe hapo ili kumpa hamu ya kula na sio kila wakati akila anakuwa peke yake. Mpe chakula akiwa na furaha na pia akiwa na njaa ili aweze kufurahia chakula chake. Kabla ya kubadilisha aina ya chakula mpe kwa siku 3-4 mfululizo ili aweze kukizoea na kama kitamletea madhara ujue hasa ni chakula gani. Usimchanganyie vyakula maana hutajua anapenda nini na kuchukia nini na pia kama kuna kitu kitamdhuru ukichanganya hautagundua kwa urahisi.
Miezi 6-9
Endelea kunyonyesha na anza kumpa vyakula vyenye madini ya chuma. Mtoto alishwe kwa ratiba inayoeleweka kila siku na katika ratiba hiyo hakikisha angalau mara moja kwa siku muda wake wa kula unakuwa sawa na muda wa familia yote ili muweze kula pamoja. Vyakula vyake viwe vimepondwapondwa kabisa ikiwezekana tumia blender na hakikisha anapata mlo kamili yani matunda, mbogamboga, mbegu, nafaka, nyama na samaki. Inashauriwa kutokuchanganya aina tofauti za nafaka kwenye unga mmoja unapomtengenezea uji, uwe na unga wa mahindi, ulezi,mchele n.k tofauti tofauti. Pika aina moja ya uji kwa wakati unaweza kufanya kwa wiki au vyovyote utakavyopenda.
 Unapompa mboga au matunda anza na tunda moja moja kwa wakati. Osha vizuri matunda yako na katakata vizuri na kuponda ponda kisha mpe kiasi kidogo kwa wakati na kikibaki usikiweke, mtengenezee kile atakachokula tu. Matunda kama papai, parachichi na embe ni mazuri kwa kuanzia. Chemsha maharage, njegere au mboga za majani na kumpa supu kidogo kidogo, usiweke chumvi nyingi kidogo sana inatosha. Usimpe juisi za madukani, hakikisha unamtengenezea juisi wewe mwenyewe na usichanganye matunda mbalimbali kwenye juisi moja, na usiweke sukari kabisa.
Miezi 9-12
Katika umri huu mtoto anakuwa tayari amezoea ladha tofauti tofauti za vyakula mbalimbali nje ya maziwa. Anauwezo wa kukaa na kushikilia kitu kwa mikono yake na kuweka mdomoni hivyo anza kumpa matunda laini mkononi aanze kujifunza kula mwenyewe. Hakikisha vipande sio vidogo sana anavyoweza kumeza ili kuepuka hatari ya kukabwa. Kwa sababu pia atakuwa ameanza kuota meno atakuwa anapenda sana kutafuna tafuna. Katika umri huu pia unaweza kuanza kumpa kiini cha yai, ute wa yai hadi afike umri wa mwaka mmoja. Endelea kumnyonyesha ila kwa sasa anakula kwanza kisha ndio ananyonya maana akinyonya sana anaweza akakataa chakula. Usimpe chakula kimoja mfululizo kwa muda mrefu maana atakinai na kuanza kukataa chakula, mpe vyakula tofauti tofauti ili aendelee kupenda chakula.
Jinsi ya Kutengeneza Chakula cha Mtoto
Ni rahisi sana kutengeneza chakula cha mtoto nyumbani kwako. Osha mikono yako vizuri kabla ya kuandaa chakula na hakikisha unatumia vyombo visafi.
Matunda na mboga mboga: osha mboga zako vizuri kwa maji safi ( ya uvugu vugu) na kisha katakata na kubandika jikoni kwa chumvi kidogo sana bila mafuta. Ikichemka isage kwenye blender au ponda ponda iwe laini kabisa kisha mpe mtoto. Matunda osha pia kwa maji ya uvugu vugu, toa ganda la nje na kata vipande vikubwa kama unataka ale kwa mikono yake mwenyewe au ponda ponda na upe kwa kijiko.
Nyama na Samaki: Chemsha vipande vya nyama na maji kidogo na iive kwa moto wa kiasi hadi ilainike kabisa kisha isage kwenye mashine (food processor) na umpe na ile supu. Samaki vile vile ila samaki hakuna haja ya kuisaga maana ikiiva inalainika sana na ni rahisi kwa mtoto kula bila taabu (Kuwa makini sana na mifupa!).
Mbegu: Hapa nazungumzia maharage, kunde, choroko, njegere n.k Pika hadi ziive kabisa na kulainika kisha pondaponda na kumpa mtoto. Pia viazi na ndizi vinafaa sana kwa watoto, unaweza ukachanganya na supu ya samaki / nyama au na maziwa.
Nafaka: Usichanganye nafaka tofauti tofauti kwa ajili ya uji wa mtoto, inashauriwa kuwa na unga tofauti kwa kila nafaka. Unapopika uji unaweza kuweka karaga zilizosagwa ili kuongeza mafuta na vitamin kwenye lishe ya mtoto.
Usalama katika Kula
  1. Hakikisha haumuachi mtoto mdogo na chakula au kinywaji bila uangalizi hata kama ni maziwa ya chupa asije akapaliwa. Usimpe mtoto chakula au maziwa akiwa amelala, analia au anacheka.
  2. Usimpe chakula ambacho kinaweza kumkaba au kumpalia kama karanga, maindi, zabibu n.k
  3. Kabla ya kumpa mtoto chakula hakikisha umekiangalia joto lake usije ukamuunguza mdomo.
  4. Usafi wa mtayarishaji, mlishaji na mlishwaji ni muhimu san asana.
Mfano wa Ratiba ya Mlo wa Mtoto
Ratiba hii ni ya mfano tu, vyakula vilivyotenganishwa na / inamaana nikimojawapo kati ya hivyo. Hakikisha vyakula havichukui nafasi ya maziwa maana ni ya muhimu kwa afya ya mtoto wako.

MUDA MIEZI 6 – 9 MIEZI 9 – 12
Alfajiri (saa 11-12) Maziwa ya mama Maziwa ya mama
Asubuhi (saa 1-2) Maziwa ya mamaUji ( Cerelac)
Tunda la kupondwa pondwa
Maziwa ya mamaUji ( Cerelac)
Tunda la kupondwa pondwa
Kabla ya mchana (saa 4-5) Maziwa /  Kipande cha mkateMaji Maziwa / andazi / chapatti laini / Kiini cha yaiMaji
Mchana (saa 6-7) Ndizi / Viazi / Wali vya kupondwa pondwaSupu ya mboga ya majani / mbegu / samaki / nyama
Tunda la kupondwa pondwa
Ndizi / Viazi / Wali / UgaliMboga za majani / Nyama / Mbegu / Samaki
Kipande cha Tunda
Alasiri ( Saa 9-10) Maji Maji
Jioni (saa 12-1) Uji / CerelacSupu ya mboga / mbegu / nyama / samaki Uji / CeleracMboga / Mbegu / Nyama / Samaki
Usiku ( muda wowote) Maziwa Maziwa

JIFUNZE KUTENGENEZA KWA UMARIDADI NA UFASAHAA KIFUA CHA KUKU




MAHITAJI
1 kijiko kidogo cha chai Kosher Salt
1 kijiko kidogo cha chai Freshly Ground Black Pepper
1 kijiko kidogo cha chai Onion Powder
1 kijiko kidogo cha chai Garlic Powder
1 kijiko kidogo cha chai Dried Parsley Flakes
Na Chef Issa Kapande
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Changanya viungo vyote kwa mara moja kisha mwagia juu ya vifua vya kuku

Ukitaka upate harufu na ladha safi toka katika viungo hivi hakikisha umeasha moto na kikaango kipate moto wa kutosha kisha mwagia mafuta yakupikia yakutosha na mwagia pia viungo vilivyobakia kwenye kikaango kisha weka hivyo vifua vyakuku na upunguze moto uwe wa wastani.

Chukua mfuniko funika ila acha wazi kiasi kama muonekano kwenye picha lengo ni kupunguza mvuke isiwe kama tunachemsha badala ya kukaanga. Kaanga kwa dakika 3 kisha geuza upande wa pili uweze pata rangi ya kahawia nzuri.
 
Baada ya kugeuza upande wa pili huu ndio muonekano wake na kisha pika pia kwa dakika 3 na kifua cha kuku kitakua kimeiva. Kumbuka unapogeuza upande wa pili toa na mfuniko usifunike tena.

Huu ni muonekano wa perfectly cooked and seasoned chicken breast baada ya kukata ndani inakua laini na ladha safi kabisa sio kau kau na kupoteza ladha.


KIfua hiki cha kuku mimi na familia yangu tulikula na mchanganyiko wa parachici, slice za vitunguu, slice za nyanya mbivu limao na giligilani mhhhhhh safi sana.
 
NDANI YA DAKIKA 10 CHAKULA TAYARI

JIFUNZE KUTENGENZA KEKI YA NDIZI MBIVU


RECIPE SAFI KABISA NA JINSI YA KUETENGENEZA KEKI YA NDIZI MBIVU

MAHITAJI
360gram unga wa ngano
180 gram sukari
1 kijiko kidogo cha chai baking powder
1/2 teaspoon baking soda
1/4 kijiko kidogo cha chai chumvi
4 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya karanga
6 ndizi za kuiva zigandishe kwenye freezer
1/2 kijiko kidogo cha chai vanilla essence
100 gram korosho au karanga za kuoka

Kwajili ya Honey Cinnamon Frosting (Sio lazima)
300 gram Icing sugar
120 gram siagi isiyo na chumvi iyeyuke kama mafuta mgando yakupaka
1 kijiko kikubwa cha chakula Asali
1/8 kijiko kidogo cha chai unga wa cinnamon (Mdarasini)
  Na Chef Issa Kapande
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI


Washa oven yako katika moto wa 350 degrees. Chukua backing tray yenye mashimo 12 ya muffin kisha weka zile karatasi maalumu za kuokea au paper liners. Chukua bakuli safi kavu kasha changanya Unga wa ngano, sukari, baking powder na chumvi salt.


Kisha toa ndizi zilizokua katika freezer ziweke nje kwa dakika 20 zitoe barafu.
 
Menya ndizi na ziweke kwenye blenda saga mpaka upate rojo safi kabisa.

Kisha mwagia mchanganyiko wako wa ndizi kwenye mchanganyiko wa unga pamoja na mafuta ya karanga na vanilla.

Tumia mwiko kuchanganya pole pole mpaka mchanganyiko wako uchanganyike vizuri.
 
Chukua kijiko kikubwa au mwiko kisha anza kumimina pole pole kwenye mashimo ya muffin.

Hakikisha umegawanya vizuri mchanganyiko wako utimie maffin 12 na ujazo uwe kama muonekano katika picha.

Oka ukiweka toothpick kati kati ya muffin na ukitoa inatoka safi bila uji uji,  kwa dakika 25 hadi 30.

Zitoe muffin zako zikiwa bado katika zile karatasi maalumu za kuokea na weka zipoe ktk wire rack.

Kwajili ya Frosting ya asali:  Kisha chukua Asali, sukari ya unga, unga wa mdarasini na siagi ilyoyeyuka kama mafuta mgando ya kupaka.

Nakushauri kutumia mixer ya umeme, piga kwadakika 4 hadi 5 mchanganyiko utakua laini.

Unaweza tumia walnut au karanga au korosho chaguo ni lako kisha zi chop chop.
 
Nakushauri tumia piping bag kupambia kwajuu. Unaweza tumia hata kijiko kupambia.
 
Sio lazima kuweka frosting lakini ukiweka inapendeza zaidi na utamu ndio unazidi na harufu safi ya mdalasini.

Mafuta ya karanga yanasaidia sana keki yako isishike na iwe rahisi kutoa wakati wa kula pia kwa wenye matatizo ya kiafya hasa sukari usitumie frosting.

Unaona vizuri spongy kwa ndani? Ipo fluffy, light and very flavorful.

We enjoyed them the day I made them (for evening tea or breakfast the next morning after warming them up slightly. It makes a great breakfast too.
 
Mwagia kwa juu hizo karanga  zitaongeza ladha safi pia


Kama mchanganyiko wako utakua mzito basi unaweza ongeza maji ya vugu vugu 60 gram usitumie maziwa yataifunika ladha ya ndizi.

RECIPE SAFI SANA YA KITAFUNWA HIKI CHENEY LADHA YA NDIZI, MDARASINI NA ASALI

JIFUNZE KUTENGENEZA ENCHILADA YA KUKU NA MAHINDI MABICHI



KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA ENCHILADA YA KUKU NA MAHINDI MABICHI PIA HISTORIA YAKE

MAHITAJI
12pc tortilla za mahindi
480 gram nyama ya kuku
480gram mahindi mabichi (sweet corn) 
480 gram shredded cheese (cheddah)
1 kopo kubwa la enchilada sauce
sour cream (Sio lazima nikwajili ya kupambia)
na chef issa Kapande
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI







JIFUNZE KUTENGENEZA PANCAKE SAFI NA NZITO KWAJILI YA KITAFUNWA



RECIPE SAFI KABISA YA PANCAKE NZITO NA SAFI KWA KITAFUNWA CHA ASUBUHI, MCHANA AU JIONI
 
MAHITAJI
240 gram unga wa ngano
3 kijiko kikubwa cha chakula sukari (white sugar)
1/2 kijiko kidogo cha chai Baking Soda
1/2 kijiko kidogo cha chai Baking Powder
1/2 kijiko kidogo cha chai chumvi
360 gram cups fresh cream
1 pc yai
kijiko kikubwa cha chakula butter  au (Siagi)
kijiko kikubwa cha chakula vanilla 
muuandaaji ni chef issa kapande
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
Chukua bakuli safi kavu kasha changanya unga wa ngano, sukari, chumvi, baking powder na baking soda.

Kisha chukua bakuli nyingine safi na kavu kasha changanya pamoja mayai, vanilla essence, siagi na fresh cream kama huna unaweza tumia maziwa badala yake.

Kisha chukua mchanganyiko wa mayai na maziwa mwagia kwenye mchanganyiko wa wa unga na koroga pole pole. Kisha weka pembeni acha kwa dakika 5 hadi 10 sio lazima lakini kama ukiweka kwa muda huo itulie pancake yako itatoka vizuri sana.

Chukua non stick pan, mwagia mafuta kiasi hakikisha jiko lako halina moto mkali au moto mdogo . Medium heat is perfect for pancakes. chukua kijiko kikubwa au upawa mmoja chota na mwagia katika kikaango.

Ukitaka kujua recipe umeipatia au jiko lako linamoto safi basi utaona  holes au bubbles zinatokea kwa juu sasa ujue ndio na muda wa kugeuza umefika igeuze pancake yako. Kawaida inachukua kama 50 sekunde mpaka dakika.

Turn the pancakes when golden brown and let it cook for another few seconds or until done.

Angalia pancake ilivyochambuka safi sana na nzito ukila unashiba

Hapa familia lazima ijiume videle bwana


Tumia kitambaa kizito au towel kuzifunika wakati unaendelea kupika ili zibaki na moto kwani zinapendeza kuliwa zikiwa za moto wakati wa kula unaweza mwagia maple syrup oooooh ladha yake itakua baabkubwa (a must! Dont even think of skipping it) and feel heaven coming down :) Pia unaweza kutumia chocolate sauce au strawberry syrup.

JIFUNZE KUAMSHA LADHA KWENYE WALI ULIOPIKWA NA UKALALA





MAHITAJI
700 gram za wali uliolala ( Kiporo)
1pc kitunguu maji kikubwa
5 pc nyanya za kuiva
1 kijiko kidogo cha chai dengu
1/4 kijiko kidogo cha chai pili pili manga
1/4 kijiko kidogo cha chai Turmeric powder
kijiko kidogo cha chai Sambar Powder, 
1 pili pili moja kavu (siolazima)
kijiko kidogo cha chai mafuta ya kupikia
kijiko kidogo cha chai siagi
Majani ya Curry kiasi
majani ya giligilani kiasi
na chef issa
KUJIFUNZA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI