mapishimapishi

mapishimapishi

Jumatatu, 17 Machi 2014

VYAKULA VINAVYOCHANGIA UKOSEFU WA USINGIZI


Kahawa.
Utafiti umethibitisha kuwepo uhusiano kati ya ukosefu wa usingizi na matatizo ya kiafya kama vile ugonjwa wa moyo, ugonjwa wa kisukari na saratani
KINACHOSABABISHA UKOSEFU WA USINGIZI
Ingawa msongo wa mawazo nao unatajwa kuchangia mtu kukosa usingizi, lakini mlo unaweza kuwa ndiyo sababu kubwa inayoweza kumkosesha mtu usingizi, na hasa vyakula vitano vifuatavyo:

Bia
POMBE
Unywaji wa bia moja ama mbili unaweza kukufanya upate usingizi haraka, hivyo kukufanya uamini kuwa pombe inasaidia mtu kupata usingizi haraka. Ingawa unaweza kupata usingizi haraka kwa kunywa pombe, lakini utafiti umeonesha kuwa usingizi huwa unakata usiku wa manane, au sehemu ya pili ya usingizi na kukuamsha asubuhi ukiwa mchovu.
KAHAWA
Inajulikana kwamba kahawa ndiyo chanzo kikuu cha kilevi aina ya ‘caffeine’. Inaelezwa kwamba kilevi hiki hudumu mwilini kwa muda usiopungua saa tano, hivyo kutegemeana na wakati gani umetumia kahawa, athari zake huweza kuonekana hadi usiku wakati wa kulala.

Hivyo kwa mtu mwingine, hasa mwenye matatizo ya usagaji chakula tumboni (poor metabolism), kikombe cha kahawa utakachokunywa mchana, athari zake zinaweza kuonekana hadi usiku wakati wa kulala, kwani unaweza kujikuta unapoteza usingizi wakati kahawa ulikunywa mchana au asubuhi.

Chokoleti nyeusi.
CHOKOLETI NYEUSI (Dark chocolate)

Ingawa chokoleti kwa kawaida, huwa na faida ya kuimarisha kinga ya mwili kwa kuwa na kiasi kingi cha virutubisho aina ya ‘antioxidant’, lakini pia ina kiwango kingi cha ‘caffeine’ ambacho kinaweza kuchangia ukosefu wa usingizi kama tayari unalo tatizo hilo.

VYAKULA VYENYE VIUNGO VINGI

Vyakula vilivyoungwa kwa viungo vingi vya aina mbalimbali, zikiwemo pilipili, huchangia tatizo la chakula kushindwa kusagika vizuri tumboni hali ambayo humfanya mtu kupata usingizi kwa tabu. Inaelezwa kuwa kirutubisho aina ya ‘capsaicin’ kinachopatikana ndani ya pilipili, huongeza joto la mwili na ndicho kinachochangia mtu kukosa usingizi.

VYAKULA VYENYE MAFUTA

Ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi pia navyo vinatajwa kuchangia ukosefu wa usingizi au usingizi wa kukatika mara kwa mara. Hivyo katika kushughulikia tatizo la kukosa usingizi usiku, huna budi kujiepusha na ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, hasa vile vya kukaanga, muda mfupi kabla ya kupanda kitandani kulala.

USITUMIE VIDONGE

Wengi wenye matatizo ya kukosa usingizi hukimbilia kumeza vidonge vya usingizi. Kitendo cha kumeza vidonge vya usingizi huwa hakiondoi tatizo, bali husogeza mbele tatizo kwa kuudanganya ubongo. Zaidi wanaotumia vidonge ili kupata usingizi, huamka wakiwa wamelewa.

DONDOO ZA KUKUSAIDIA KUPATA USINGIZI

Kabla ya kulala, kunywa glasi ya maziwa moto au ya uvuguvugu. Au kula karanga au siagi ya karanga (peanut butter). Au kula zabibu kadhaa. Vyakula hivyo, ingawa vipo na vingine vingi, vinatajwa kuwa na virutubisho vinavyozalisha homoni za usingizi kwa wingi.

Aidha, kwa wenye matatizo ya kukosa usingizi kwa muda mrefu, wanashauriwa kulala kwenye chumba chenye giza kabisa, kujiepusha na kuangalia TV wakiwa wamelala kitandani, kulala mbali na simu, redio, saa na vitu vingine vyenye sumaku. Vitu hivi vimeonekana kuharibu mtiririko wa usingizi kwa njia moja au nyingine hivyo kwa mtu mwenye matatizo ya kukosa usingizi akaenavyo mbali.

Alhamisi, 13 Machi 2014

FAHAMU MAGONJWA YANAYOWEZA KUTIBIKA KWA KULA NDIZI


  Ndizi ni aina ya tunda linalopendwa na watu wengi yawezekana huwa unakula tunda hili bila kujua faida zake, lakini pia yawezekana wewe hupendi kabisa kula ndizi mbivu, lakini ni vyema kufahamu kuwa tunda hili ni muhimu sana kwa afya yako inasaidia kama wewe hujapatwa na vidonda vya tumbo, kwa kula ndizi mara kwa mara unajipa kinga madhubuti na kama tayari umeathirika na vidonda, kwa kula ndizi utajipa ahueni kubwa.


Kwa mujibu wa utafiti wa kisayansi kuhusu tunda hili, ndizi ni chanzo kikubwa cha madini aina ya ‘Potassium’, ambayo ni muhimu sana katika kuweka shinikizo la damu mwilini katika hali yake ya kawaida (Normal Blood Pressure), na huboresha utendajikazi mzuri wa moyo. Ndizi moja tu kwa siku inaweza kukukinga na maradhi ya shinikizo la damu na matatizo ya moyo.

Jumapili, 9 Machi 2014

Muujiza ya matibabu kwa maji ya moto kunywa magonjwa yanatibiwa na maji ya moto


 


 Click image for larger version. 

Name: warm_water.jpg 
Views: 0 
Size: 13.7 KB 
ID: 143690
- pumu= asthma

- shinikizo la damu= hbp 


- migraine / kichwa= migraine/ headache


- ugonjwa wa sukari= diabetes 


- upungufu wa damu= anemia


- maumivu nyuma= back pain


- mawe katika figo= urinary calculus 


- maambukizo wa haja ndogo= urinary tract infection 


- cholesterol= cholesterol


- baridi yabisi & ugonjwa wa mifupa= rheumatism & arthritis 


- kiharusi =stroke 


- udhaifu wa mwili =sexual and body weakness


- kuchoka & uchovu = tiredness & fatigue


- tonsili =tonsillitis 


- vijidudu vya tumbo = gastroenteritis (stomach virus)


- mafua/homa =colds, flu & fever 


- kukosa usingizi= insomnia (lack of sleep) 


- kichome kwenye roho= heartburn 



- kidonda tumboni =stomach ulcer


- kuvimbiwa (ugumu kupata haja kubwa) =constipation


- kutetemeka mwili kutokana na umri= parkinsonism 


- kupoteza nywele (upaa) =hair loss (baldness)


- magonjwa ya ngozi=skin diseases (psoriasis)


- kasoro ya ubongo =alzheimer (defects of the brain) 


- maradhi ya moyo =heart disease 


- saratani= cancer 


- usafisha heidh ya kila mwezi ya wanawake= purifying women's monthly period
Click image for larger version. 

Name: warm_water.jpg 
Views: 0 
Size: 13.7 KB 
ID: 143690

Jumamosi, 8 Machi 2014

JIFUNZE KUTENGENEZA KITAFUNWA HIKI CHA KARANGA NA CHOCOLATE

KAA TAYARI KWA MAELEZO YA VYAKULA VYOTE AMBAVYO HAVINA MAELEZO HAPO CHINI.
PIA NITAKUPATIA RECIPE SAFI KABISA YA KITAFUNWA HIKI CHA KARANGA NA CHOCOLATE

MAHITAJI
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI













UNAZIJUA TABLE MANNERS WAKATI WA KULA?HIZI HAPA ZISOME

 
Hivi ni chache nazovikumbuka tuongeze mingine

1. Tafuna ukiwa umefunga mdomo

2. Usiongee ukiwa na chakula mdomoni

3. Usipitishe mkono/mikono juu ya chakula cha mwingine.

4. Usiongeze chumvi au pilipili kabla hujaonja chakula

5. Unapokunywa supu kijiko cha supu hakitakiwi kuingizwa mdomoni, supu hunywewa toka kona ya kijiko.

Top Ten Table Manners

Keep these basic behaviors in mind as you eat:

1. Chew with your mouth closed.
2. Avoid slurping, smacking, blowing your nose, or other gross noises. (If necessary, excuse yourself to take care of whatever it is you need to take care of.)
3. Don’t use your utensils like a shovel or as if you’ve just stabbed the food you’re about to eat.
4. Don’t pick your teeth at the table.

5. Remember to use your napkin at all times.
6. Wait until you’re done chewing to sip or swallow a drink. (The exception is if you’re choking.)
7. Cut only one piece of food at a time.
8. Avoid slouching and don’t place your elbows on the table while eating (though it is okay to prop your elbows on the table while conversing between courses.)
9. Instead of reaching across the table for something, ask for it to be passed to you.
10. Always say ‘excuse me’ whenever you leave the table.