
Kahawa.
Utafiti 
umethibitisha kuwepo uhusiano kati ya ukosefu wa usingizi na matatizo ya
 kiafya kama vile ugonjwa wa moyo, ugonjwa wa kisukari na saratani
KINACHOSABABISHA UKOSEFU WA USINGIZI
Ingawa 
msongo wa mawazo nao unatajwa kuchangia mtu kukosa usingizi, lakini mlo 
unaweza kuwa ndiyo sababu kubwa inayoweza kumkosesha mtu usingizi, na 
hasa vyakula vitano vifuatavyo:
POMBE
Unywaji 
wa bia moja ama mbili unaweza kukufanya upate usingizi haraka, hivyo 
kukufanya uamini kuwa pombe inasaidia mtu kupata usingizi haraka. Ingawa
 unaweza kupata usingizi haraka kwa kunywa pombe, lakini utafiti 
umeonesha kuwa usingizi huwa unakata usiku wa manane, au sehemu ya pili 
ya usingizi na kukuamsha asubuhi ukiwa mchovu.
KAHAWA
Inajulikana
 kwamba kahawa ndiyo chanzo kikuu cha kilevi aina ya ‘caffeine’. 
Inaelezwa kwamba kilevi hiki hudumu mwilini kwa muda usiopungua saa 
tano, hivyo kutegemeana na wakati gani umetumia kahawa, athari zake 
huweza kuonekana hadi usiku wakati wa kulala.
Hivyo 
kwa mtu mwingine, hasa mwenye matatizo ya usagaji chakula tumboni (poor 
metabolism), kikombe cha kahawa utakachokunywa mchana, athari zake 
zinaweza kuonekana hadi usiku wakati wa kulala, kwani unaweza kujikuta 
unapoteza usingizi wakati kahawa ulikunywa mchana au asubuhi.

Chokoleti nyeusi.
CHOKOLETI NYEUSI (Dark chocolate)
Ingawa 
chokoleti kwa kawaida, huwa na faida ya kuimarisha kinga ya mwili kwa 
kuwa na kiasi kingi cha virutubisho aina ya ‘antioxidant’, lakini pia 
ina kiwango kingi cha ‘caffeine’ ambacho kinaweza kuchangia ukosefu wa 
usingizi kama tayari unalo tatizo hilo.
VYAKULA VYENYE VIUNGO VINGI
Vyakula 
vilivyoungwa kwa viungo vingi vya aina mbalimbali, zikiwemo pilipili, 
huchangia tatizo la chakula kushindwa kusagika vizuri tumboni hali 
ambayo humfanya mtu kupata usingizi kwa tabu. Inaelezwa kuwa kirutubisho
 aina ya ‘capsaicin’ kinachopatikana ndani ya pilipili, huongeza joto la
 mwili na ndicho kinachochangia mtu kukosa usingizi.
VYAKULA VYENYE MAFUTA
Ulaji wa 
vyakula vyenye mafuta mengi pia navyo vinatajwa kuchangia ukosefu wa 
usingizi au usingizi wa kukatika mara kwa mara. Hivyo katika 
kushughulikia tatizo la kukosa usingizi usiku, huna budi kujiepusha na 
ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, hasa vile vya kukaanga, muda mfupi
 kabla ya kupanda kitandani kulala.
USITUMIE VIDONGE
Wengi 
wenye matatizo ya kukosa usingizi hukimbilia kumeza vidonge vya 
usingizi. Kitendo cha kumeza vidonge vya usingizi huwa hakiondoi tatizo,
 bali husogeza mbele tatizo kwa kuudanganya ubongo. Zaidi wanaotumia 
vidonge ili kupata usingizi, huamka wakiwa wamelewa.
DONDOO ZA KUKUSAIDIA KUPATA USINGIZI
Kabla ya 
kulala, kunywa glasi ya maziwa moto au ya uvuguvugu. Au kula karanga au 
siagi ya karanga (peanut butter). Au kula zabibu kadhaa. Vyakula hivyo, 
ingawa vipo na vingine vingi, vinatajwa kuwa na virutubisho 
vinavyozalisha homoni za usingizi kwa wingi.
Aidha,
 kwa wenye matatizo ya kukosa usingizi kwa muda mrefu, wanashauriwa 
kulala kwenye chumba chenye giza kabisa, kujiepusha na kuangalia TV 
wakiwa wamelala kitandani, kulala mbali na simu, redio, saa na vitu 
vingine vyenye sumaku. Vitu hivi vimeonekana kuharibu mtiririko wa 
usingizi kwa njia moja au nyingine hivyo kwa mtu mwenye matatizo ya 
kukosa usingizi akaenavyo mbali.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni